HomeRadio Vaticana
foto testata  

Categories


  Charity & Solidarity


  Church


  Culture & Society


  Vatican Documents


  Synod


  Ecumenism


  Family


  Youth


  Justice & Peace


  Politics


  Religion & Dialogue


  Science & Ethics


  Audiences
   & Angelus



  Pastoral visits


cx_t01

CTV - You tube

CTV



 home > Charity & Solidarity  > news


04/11/2009 8.54.53



Ulimwengu wa utandawazi ni changamoto ya Uinjilishaji mpya unaohitaji mikakati mipya ya kichungaji






Askofu mkuu Agostino Marchetto, Katibu mkuu wa Baraza la Kipapa la Shughuli za kichungaji kwa ajili ya wakimbizi, wahamiaji na watu wasiokuwa na makazi maalum anasema, Kongamano la sita la kimataifa kwa ajili ya wahamiaji na wakimbizi linalenga kupembua kwa kina changamoto zinazoendelea kujitokeza katika ulimwengu wa utandawazi, miaka mitano baada ya kuchapisha hati ya kichungaji kuhusu wakimbizi na wahamiaji.

Kongamano hili litakuwa ni fursa kwa viongozi wa Kanisa, wanasiasa na mashirika ya kimataifa yanayotoa huduma zao kwa wakimbizi na wahamiaji kushirikishana mang'amuzi na changamoto zinazojitokeza katika ulimwengu wa utandawazi, ili kutoa jibu muafaka kwa changamoto hizi mintarafu tunu msingi za maisha ya Kiinjili.

Askofu mkuu Marchetto akizungumza na waandishi wa habari, siku ya jumanne, tarehe 3 Oktoba, 2009, wakati Baraza la Kipapa lilipokuwa linafafanua juu ya ratiba ya matukio makuu kuhusu Kongamano la sita la Kimataifa kwa ajili ya wakimbizi na wahamiaji. Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita aliwahi kusema kwamba, ulimwengu wa utandawazi ni changamoto kubwa katika Uinjilishaji mpya pamoja na mikakati mipya ya shughuli za kichungaji.


  « back to index

 






05/11/2009 9.12.28
Tatizo la wakimbizi na wahamiaji linapaswa kushughulikiwa kimataifa ili kupata ufumbuzi wa kudumu


04/11/2009 9.14.03
Viongozi wa Kanisa, Mashirika ya Kimataifa, Wanasiasa na Wanadiplomasia ni kati ya washiriki wakuu wa Kongamano la sita kwa ajili ya wahamiaji na wakimbizi


04/11/2009 8.42.16
Upendo wa Kristo unalibidisha Kanisa kuwajali na kuwasaidia wakimbizi na wahamiaji


03/11/2009 13.50.43
Kongamano la sita la wakimbizi na wahamiaji kimataifa kufunguliwa rasmi tarehe 9 Novemba, 2009


03/11/2009 8.57.43
"Iweni mfano mwema katika ujenzi wa Burundi mpya katika misingi ya upatanisho, haki na amani"



Related categories


Page précédente  Previous page
Page d'accueil  Home Page
Ecrire à la rédaction  Contact us
top
top
All the contents on this site are copyrighted ©. Webmaster / Credits / Legal Conditions
top
top