HomeRadio Vaticana
foto testata  

Categories


  Charity & Solidarity


  Church


  Culture & Society


  Vatican Documents


  Synod


  Ecumenism


  Family


  Youth


  Justice & Peace


  Politics


  Religion & Dialogue


  Science & Ethics


  Audiences
   & Angelus



  Pastoral visits


cx_t01

CTV - You tube

CTV



 home > Charity & Solidarity  > news


04/11/2009 9.14.03



Viongozi wa Kanisa, Mashirika ya Kimataifa, Wanasiasa na Wanadiplomasia ni kati ya washiriki wakuu wa Kongamano la sita kwa ajili ya wahamiaji na wakimbizi






Monsinyo Novatus Rugambwa, Katibu mkuu msaidizi wa Baraza la Kipapa la shughuli za kichungaji kwa ajili ya wahamiaji, wakimbizi na watu wasiokuwa na makazi maalum, akizungumza na waandishi wa habari siku ya jumanne, tarehe 3 Novemba, 2009 kuhusu Kongamano la sita la kimataifa kwa ajili ya wakimbizi na wahamiaji anasema, hii itakuwa ni fursa ya kuweza kusikiliza mang'amuzi na changamoto kutoka kwa wazungumzaji kumi na nne walioalikwa rasmi na Baraza lao.

Kongamano hili linahudhuriwa na Maaskofu hamsini na tatu wanaohusika kwa karibu zaidi na huduma kwa wakimbizi, wahamiaji na watu wasiokuwa na makazi. Mapadre hamsini na saba, watawa kumi na sita na walei kumi na tisa watarajiwa kushiriki. Jumla ya wawakilishi kutoka Mabaraza ya Maaskofu Katoliki watakuwa ni mia moja na arobaini na nne. Mashirika ya kitawa yatawakilishwa kikamilifu kwani hawa wamekuwa mstari wa mbele katika utoaji wa huduma kwa wahamiaji, wakimbizi na watu wasiokuwa na makazi maalum.

Monsinyo Novatus Rugambwa anaendelea kubaini kwamba, Kongamano la sita la kimataifa, litayashirikisha pia mashirika ya kimataifa kutoka Umoja wa Mataifa, Mashirika ya Kimataifa ya Huduma kutoka Kanisa Katoliki pamoja na wataalam, kwa pamoja watashirikiana bega kwa bega na Baraza hili la Kipapa, ili kufanikisha Kongamano hili.

Mabalozi kadhaa wanaowakilisha nchi zao mjini Vatican wanatarajiwa pia kuhudhuria. Kimsingi anasema Monsinyo Rugambwa ni kwamba, kutakuwa na watu mia tatu na ishirini wanaotarajiwa kuhudhuria Kongamano la sita la kimataifa kwa ajili ya wakimbizi na wahamiaji katika ulimwengu wa utandawazi.


  « back to index

 






06/11/2009 12.32.30
The Holy See at the UN: Renewable energy is the key to poverty eradication.


05/11/2009 9.12.28
Tatizo la wakimbizi na wahamiaji linapaswa kushughulikiwa kimataifa ili kupata ufumbuzi wa kudumu


04/11/2009 8.54.53
Ulimwengu wa utandawazi ni changamoto ya Uinjilishaji mpya unaohitaji mikakati mipya ya kichungaji


04/11/2009 8.42.16
Upendo wa Kristo unalibidisha Kanisa kuwajali na kuwasaidia wakimbizi na wahamiaji


03/11/2009 13.50.43
Kongamano la sita la wakimbizi na wahamiaji kimataifa kufunguliwa rasmi tarehe 9 Novemba, 2009



Related categories


Page précédente  Previous page
Page d'accueil  Home Page
Ecrire à la rédaction  Contact us
top
top
All the contents on this site are copyrighted ©. Webmaster / Credits / Legal Conditions
top
top