HomeRadio Vaticana
foto testata  

Categories


  Charity & Solidarity


  Church


  Culture & Society


  Vatican Documents


  Synod


  Ecumenism


  Family


  Youth


  Justice & Peace


  Politics


  Religion & Dialogue


  Science & Ethics


  Audiences
   & Angelus



  Pastoral visits


cx_t06

CTV - You tube

CTV



 home > Church > news


07/11/2009 9.44.36



Michezo ni sehemu ya utangazaji wa Habari Njema na Majiundo ya kimaadili na kiutu






Kardinali Stanslaw Rylko, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya walei anasema, imani inaweza kuleta mwelekeo mpya katika katika shughuli za michezo na utamaduni. Michezo kwa miaka mingi imekuwa ni sehemu muhimu kwa ajili ya majiundo ya vijana duniani, jambo ambalo linaungwa mkono pia na Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican kama njia ya kuboresha tunu msingi za maisha adili na kiutu.

Idara ya michezo ya Baraza la Kipapa kwa ajili ya walei, limeandaa semina maalum inayoongozwa na mada: michezo, elimu na imani, mwelekeo mpya katika shughuli za michezo ndani ya Kanisa Katoliki. Lengo la semina hii ni kuwawezesha wahusika kutambua uhusiano uliopo kati ya michezo, majiundo ya binadamu na imani mintarafu vyama vya michezo vinavyosimamiwa na kuongozwa na Kanisa Katoliki.

Kardinali Ryliko anasema, hata katika michezo Kanisa bado linaendelea kutoa mchango wake wa dhati kama sehemu ya Uinjilishaji na majiundo endelevu ya mwanadamu. Hii ni mara ya tatu kwa Baraza la Kipapa kwa ajili ya walei kuandaa semina inayohusu Kanisa na michezo.

Michezo inapaswa kupewa umuhimu wake ndani ya Kanisa na kamwe isionekane kuwa ni sekta inayotishia maisha na utume wa Kanisa, lakini michezo ina mvuto wa pekee kwa vijana hata katika maisha na utume wao ndani ya Kanisa. Baadhi ya wazazi wanachukulia fursa ya michezo kama sehemu ya burudani kwa vijana hasa baada ya pilika pilika za maisha ya shule na kazi.

Lakini wengine wana maono tofauti kwani, kwa wazazi wenye watoto wenye vipaji katika michezo ni nafasi kwa watoto hao kupata umaarufu kwa siku za usoni, hali inayokwenda sambamba na ubora wa maisha. Kardinali Rylko anasema, Mama Kanisa anapaswa kuendelea kutoa msukumo wa pekee katika shughuli za michezo kama njia ya utangazaji wa Habari Njema na majiundo ya mwanadamu. Imani ikimwilishwa katika michezo inaleta utofauti katika matukio haya.


  « back to index

 






07/11/2009 11.50.00
Upendo kwa Kristo na Kanisa lake ujidhihirishe katika huduma kwa maskini


07/11/2009 10.05.47
Kanisa laomba nafasi zaidi katika matumizi ya njia za mawasiliano ya jamii Cuba


07/11/2009 8.45.06
Mama Kanisa anatoa changamoto kwa waamini kuwa wakarimu kwa Mungu na jirani


06/11/2009 10.58.36
Mh. Padre Sandri ateuliwa kuwa Askofu mpya waJimbo la Witbank


05/11/2009 18.17.53
Pope Prays for Departed Cardinals and Bishops



Related categories


Page précédente  Previous page
Page d'accueil  Home Page
Ecrire à la rédaction  Contact us
top
top
All the contents on this site are copyrighted ©. Webmaster / Credits / Legal Conditions
top
top